Timothy Kaberia
Timothy Kaberia alijiunga na Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika mwaka 2008. Mzaliwa wa Kenya, Kaberia alisomea siasa na lugha nchini ya Kenya na Marekani. Kabla ya kujiunga na Sauti ya Amerika, Kaberia alikuwa mratibu wa habari katika chuo kikuu cha American University, Washington, D.C. Alianza kazi ya utafiti na uandishi katika Tume ya Haki binadamu ya Kenya (KHRC) na baadaye akajiunga na kituo cha televisheni na redio cha Citizen mjini Nairobi kama ripota. Pia aliwahi kuwa mfasiri wa mashirika mbalimbali ikiwa ni pamoja ni kituo cha sheria na Amnesty International. Kaberia alipokea shahada ya BA (Honors) kutoka chuo kikuu cha Moi, Kenya. Alipokea mafunzo ya uandishi na mawasiliano nchini Burkina Faso na Marekani. Baadaye alipata shahada za juu katika uhusiano wa masuala ya kimataifa katika chuo kikuu cha American University mjini Washington, D.C.
|