Tuzo zilizolipwa
Mpango wa Tuzo kwa Haki umelipa zaidi ya dola milioni 100 kwa watu zaidi ya 60 ambao walitoa taarifa iliyozuia mashambulizi ya magaidi wa kimataifa au imesaidia kuwafikisha mbele ya sheria waliohusika na vitendo vya awali.
Kutokana na taarifa hii, watu wafuatao ni miongoni mwa wengine wengi wamefikishwa mbele ya sheria:
Uday Hussein
Qusay Hussein
Ramzi Ahmed Yousef
Mir Aimal Kansi
Hamsiraji Marusi Sali
Toting Craft Hanno
Muhsin Khadr al-Khafaji
Khamis Sirhan al-Muhammad
Muhammad Zimam Abd al-Razzaq al-Sadun
Khadaffy Janjalani
Abu Solaiman
Edgar Navarro
Watu majasiri waliokuwa na nia walijitokeza kwa taarifa ambazo pia zimesaidia kuzuia na kutatua mashambulizi ya kigaidi:
- Wakati wa vita vya Ghuba, mtoa habari jasiri kutoka nchi ya Mashariki mwa Asia alijitokeza mbele na habari za kushtusha kuhusu mfululizo wa mashambulizi yaliyopangwa ya kigaidi. Magaidi walikuwa tayari wamekagua maeneo waliyokusudia na waliweka pamoja silaha zenye kujiendesha zenyewe (automatik), magruneti na milipuko. Saa 48 tu kabla ya shambulizi la kwanza kati ya mashambulizi yaliyopangwa, mtoa habari alifichua habari muhimu ambazo zilizuia mpango wa magaidi. Shambulizi lilisimamishwa, kijana alipewa tuzo kubwa, na familia yake ilihamishiwa sehemu salama. Kwa kutoa habari mtu huyu ameokoa maisha ya mamia ya watu.
- Katika kesi nyingine, msichana alijitokeza na habari kuhusu watu walioiteka ndege na kuwapiga kikatili abiria waliokuwa ndani. Alieleza kuwa"alihisi lazima haki itendeke." Kiongozi wa wateka nyara alirudishwa Marekani na kufungwa kwa mashtaka ya uharamia wa ndege. Msichana alipewa tuzo kwa jitihada za kupiga vita ugaidi.
- Msichana mwingine mwanafunzi katika chuo cha kigeni, alishuhudia mauaji ya kikatili ya mwanadiplomasia wa Marekani. Kutokana na habari alizozitoa, washambuliaji wawili wamehukumiwa kifungo cha maisha. Mwanafunzi na familia yake walihamishwa kwenye makao salama na alipokea tuzo kubwa.