VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

11 Januari 2009 

Leo VOA:

Habari katika Lugha 45
Wakimbizi Wakabiliwa na Hali Ngumu Kenya

23/12/2008

A Kenyan child waits for rations near food distribution point at IDP camp near Kenya's lakeside town of Naivasha, 28 Feb 2008
Mtoto akisubiri mgao wa chakula katika kambi ya wakimbizi nchini Kenya
Maelfu ya wakimbizi waliolazimishwa kuyakimbia makazi yao wakati wa machafuko yaliyofuatia uchaguzi wa rais nchini Kenya, wanakabiliwa na hali mbaya ya maisha, licha ya serikali ya nchi hiyo kuanzisha mpango wa kuwarudisha makwao. 

Mmoja wa wakimbizi hao, Mase Wangui aliiambia Sauti ya Amerika kuwa hali ni mbaya katika makambi yao kiasi kwamba wanalazimika kujisaidia katika mifuko ya karatasi kutokana na kufurika kwa vyoo. 

Wangui anasema hali hiyo imepelekea magonjwa ya aina mbalimbali na vifo katika makambi hayo, na kwamba kina mama wajawazito wanalazimika kujifungua katika mazingira magumu mno. Anasema hata kama msaada wa serikali utatolewa, huenda watu wengine zaidi watakuwa wamepoteza maisha. 

Hali hiyo imepelekea mashirika yasiyokuwa ya kiserikali kukosoa vikali mpango wa serikali ya Kenya wa kuwarudisha wakimbizi makwao au kuwapatia makazi mapya.


Listen to This Report Bonyeza hapa kusikiliza
Fungua  (MP3)
Listen to This Report Bonyeza hapa kusikiliza
Sikiliza (MP3)
E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala mepya

  Mahojiano zaidi