VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

15 Januari 2009 

Leo VOA:

Habari katika Lugha 45
Wakenya Waandamana Kupinga Mashambulio ya Israel

09/01/2009

A supporter of Kenya's Opposition leader Raila Odinga taunts a Kenyan policeman during a demonstration in the street of Kisumu, Kenya, 16 Jan 2008
Polisi akiwazuwia vijana kufanya maandamano Kenya
Maandamano yamefanyika kuelekea ubalozi wa Israel mjini Nairobi Kenya, kupinga mashambulizi yanayofanywa na majeshi ya Israel Ukanda wa Gaza. Maandamano hayo yalianza karibu na ofisi ya Waziri Mkuu na majengo ya bunge, na kuelekea ubalozi wa Israel. 

Polisi waliokuwa katika magari maalum ya kutawanya waandamanaji walifanikiwa kuwatawanya vijana wa kiislam waliokuwa njiani kuelekea ubalozi wa Israel. Vijana hao wanaitaka serikali kumfukuza balozi wa Israel nchini Kenya, kutokana na kuhusika kwa nchi yake katika vita Ukanda wa Gaza. 

Licha ya polisi kufanikiwa kuwatawanya waandamanaji hao, vijana hao wa Kenya wameahidi kuendelea na maandamano yao hadi pale serikali ya Israel itakapokuwa imekomesha mashambulio yake Gaza.


Listen to This Report Kenya Demos
Fungua  (MP3)
Listen to This Report Kenya Demos
Sikiliza (MP3)
E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala mapya

  Mahojiano zaidi