VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

11 Januari 2009 

Leo VOA:

Habari katika Lugha 45
DRC: Mahojiano na Jenerali Nkunda


08/01/2009

Rebel General Laurent Nkunda (C) walks in the courtyard of a house after speaking with the press in the town of Kitshoumba, 02 Nov 2008
Kiongozi wa waasi wa DRC, Jenerali Laurent Nkunda
Rais wa zamani wa Nigeria Olusegun Obasanjo, ambaye pia ni mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, amewasili nchini humo ambapo anatazamiwa kukutana na rais Joseph Kabila, na kiongozi wa kundi la waasi wa CNDP, jenerali Laurent Nkunda.

Akizungumza na Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika kutoka mji wa Bunagana Alhamis, Jenerali Nkunda alisema anategemea kuwa mazungumzo baina yake na bwana Obasanjo yatampa uelewa zaidi mjumbe huyo wa Umoja wa Mataifa, kuhusu mtafaruku wa Congo. 

Jenerali huyo alisema pindi wapatanishi wa mzozo wa Congo watakapo uelewa mtafaruku huo, wataweza kutanzua vyema maswala yanayozungumziwa katika mkutano unaoendelea mjini Nairobi nchini Kenya.


Listen to This Report DRC-Nkunda
Fungua  (MP3)
Listen to This Report DRC-Nkunda
Sikiliza (MP3)
E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala mapya

  Mahojiano zaidi