VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

11 Januari 2009 

Leo VOA:

Habari katika Lugha 45
Nkunda: Hakuna Mgawanyiko Ndani ya CNDP


06/01/2009

Rebel General Laurent Nkunda (C) walks in the courtyard of a house after speaking with the press in the town of Kitshoumba, 02 Nov 2008
Kiongozi wa kundi la waasi wa CNDP, Jenerali Laurent Nkuda
Kiongozi wa kundi la waasi wa CNDP wanao pigana na majeshi ya serikali mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, amekanusha madai kuwa kuna mgawanyiko ndani ya kundi hilo. 

Akiongea na Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika leo (Jumatatu), Jenerali Laurent Nkunda amesema yeye bado ni kiongozi wa kundi hilo, na kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kuleta mgawanyiko ndani ya kundi hilo. 

Msemaji wa mkuu wa majeshi ya waasi, Jenerali Bosco Ntaganda, amekaririwa akisema kuwa makamanda walimfukuza jana Nkunda kutokana na uongozi mbaya. Lakini Nkunda amekanusha nakusema kuwa Ntaganda siyo msemaji wa CNDP au mwenyekiti. 

Aidha Jenerali Nkunda amesema mazungumzo ya amani ya Nairobi yanaendelea vizuri licha ya vipingamizi vya hapa na pale.

 


Listen to This Report Drc Nkunda
Fungua  (MP3)
Listen to This Report Drc Nkunda
Sikiliza (MP3)
E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala mepya

  Mahojiano zaidi